Zaburi 107:4-7
4
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.