Skip to content
Zaburi 107:35-41

Zaburi 107:35-41

35
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options