Zaburi 107:10-12
10
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.