Zaburi 106:7-12
7
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
Settings