Zaburi 105:28-32
28
Alituma giza na nchi ikajaa giza, kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
29
Aligeuza maji yao kuwa damu, ikasababisha samaki wao kufa.
30
Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
31
Alisema, yakaja makundi ya mainzi, na viroboto katika nchi yao yote.
32
Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe, yenye umeme wa radi nchini yao yote,
Settings