Skip to content
Zaburi 104:1-9

Zaburi 104:1-9

1
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options