ഉള്ളടക്കത്തിലേക്ക് പോകുക
Zaburi 102:11-28

Zaburi 102:11-28

11
Siku zangu ni kama kivuli cha jioni, ninanyauka kama jani.
12
Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele, sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.
13
Utainuka na kuihurumia Sayuni, kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema; wakati uliokubalika umewadia.
14
Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako, vumbi lake lenyewe hulionea huruma.
15
Mataifa wataogopa jina la Bwana, wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.
16
Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni na kutokea katika utukufu wake.
17
Ataitikia maombi ya mtu mkiwa, wala hatadharau hoja yao.
18
Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho, ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:
19
“Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu, kutoka mbinguni alitazama dunia,
20
kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”
21
Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu,
22
wakati mataifa na falme zitakapokusanyika ili kumwabudu Bwana.
23
Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu, akafupisha siku zangu.
24
Ndipo niliposema: “Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu; miaka yako inaendelea vizazi vyote.
25
Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia, nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.
26
Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu, zote zitachakaa kama vazi. Utazibadilisha kama nguo nazo zitaondoshwa.
27
Lakini wewe, U yeye yule, nayo miaka yako haikomi kamwe.
28
Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako; wazao wao wataimarishwa mbele zako.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options