Zaburi 10:1-5
1
Kwa nini, Ee Bwana, unasimama mbali? Kwa nini unajificha wakati wa shida?
2
Katika kiburi chake, mwovu humtesa maskini, waovu na wanaswe katika hila wanazozitunga.
3
Hujivunia tamaa za moyo wake; humbariki mlafi na kumtukana Bwana.
4
Katika kiburi chake, mwovu hamtafuti Mungu, katika mawazo yake yote hakuna nafasi ya Mungu.
5
Njia zake daima hufanikiwa; hujivuna na amri zako ziko mbali naye, huwacheka kwa dharau adui zake wote.
Settings