Mithali 8:32-36
32
“Basi sasa wanangu, nisikilizeni; heri wale wanaozishika njia zangu.
33
Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima; msiyapuuze.
34
Heri mtu yule anisikilizaye mimi, akisubiri siku zote malangoni mwangu, akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu.
35
Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana.
36
Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”
Settings