Mithali 8:18-21
18
Utajiri na heshima viko kwangu, utajiri udumuo na mafanikio.
19
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
20
Natembea katika njia ya unyofu katika mapito ya haki,
21
nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.