Mithali 7:21-27
21
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
22
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
23
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
24
Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
25
Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
26
Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
27
Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.
Settings