Mithali 7:18-23
18
Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
19
Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
20
Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
21
Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
22
Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
23
mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
Settings