Skip to content
Mithali 11:1-8

Mithali 11:1-8

1
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options