Wafilipi 2:17-18
17
Lakini hata kama nikimiminwa kama sadaka ya kinywaji kwenye dhabihu na huduma itokayo katika imani yenu, mimi ninafurahi na kushangilia pamoja nanyi nyote.
18
Vivyo hivyo, ninyi nanyi imewapasa kufurahi na kushangilia pamoja nami.