Skip to content
Hesabu 27:7-11

Hesabu 27:7-11

7
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
11
Ikiwa baba yake hakuwa na ndugu wa kiume, toa urithi wake kwa ndugu wa karibu katika ukoo wake, ili aumiliki. Hili litakuwa dai la sheria kwa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru Mose.’ ”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options