Hesabu 27:6-10
6
naye Bwana akamwambia Mose,
7
“Wanachosema binti za Selofehadi ni sawa. Ni lazima kwa hakika uwape milki kama urithi miongoni mwa ndugu za baba yao, na kubadili urithi wa baba yao uwe wao.
8
“Waambie Waisraeli, ‘Ikiwa mtu atakufa naye hakuacha mwana, utampa binti yake urithi wake.
9
Ikiwa hana binti, wape ndugu zake wa kiume urithi wake.
10
Ikiwa hana ndugu wa kiume toa urithi wake kwa ndugu za baba yake.
Settings