Skip to content
Hesabu 10:11-16

Hesabu 10:11-16

11
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
12
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
13
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
14
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options