Skip to content
Mika 5:10-15

Mika 5:10-15

10
“Katika siku ile,” asema Bwana, “nitaangamiza farasi zenu katikati yenu na kubomoa magari yenu ya vita.
11
Nitaiangamiza miji ya nchi yenu na kuziangusha chini ngome zenu zote.
12
Nitaangamiza uchawi wenu na hamtapiga tena ramli.
13
Nitaangamiza vinyago vyenu vya kuchonga na mawe yenu ya ibada yatoke katikati yenu; hamtasujudia tena kazi ya mikono yenu.
14
Nitangʼoa nguzo za Ashera katikati yenu na kubomoa miji yenu.
15
Nitalipiza kisasi kwa hasira na ghadhabu juu ya mataifa ambayo hayajanitii.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options