Skip to content
Mathayo 27:50-51

Mathayo 27:50-51

50
Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.

Kifo na Matukio Yaliyofuata Mara Moja

51
Wakati huo huo pazia la Hekalu likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka.

See also

Where else Scripture says this.

  • Waebrania 10:19

    Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu,
    from verse 51
  • Waebrania 10:22

    sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi.
    from verse 51
  • Marko 15:38

    Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili kuanzia juu hadi chini.
    from verse 51
  • Waebrania 6:19

    Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho iliyo imara na thabiti. Tumaini hili huingia katika sehemu takatifu iliyopo nyuma ya pazia,
    from verse 51
  • Luka 23:45

    kwa sababu jua liliacha kutoa nuru. Pazia la Hekalu likachanika vipande viwili.
    from verse 51
  • Ufunuo 11:19

    Ndipo hekalu la Mungu lililoko mbinguni likafunguliwa, na sanduku la agano lake likaonekana humo ndani. Kukatokea mianga ya umeme wa radi, ngurumo, sauti za radi, tetemeko la nchi na mvua kubwa ya mawe.
    from verse 51
  • Kutoka 26:31

    “Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
    from verse 51
  • Kutoka 26:37

    Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.
    from verse 51
  • Yohana 19:30

    Baada ya kuionja hiyo siki, Yesu akasema, “Imekwisha.” Akainamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.
    from verse 50
  • Mathayo 27:54

    Basi yule jemadari na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, waliogopa, wakasema, “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
    from verse 51
  • Isaya 53:9

    Wakamfanyia kaburi pamoja na waovu, pamoja na matajiri katika kifo chake, ingawa hakutenda jeuri, wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
    from verse 50
  • Isaya 53:12

    Kwa hiyo nitamgawia sehemu miongoni mwa wakuu, naye atagawana nyara pamoja na wenye nguvu, kwa sababu aliyamimina maisha yake hadi mauti, naye alihesabiwa pamoja na wakosaji. Kwa kuwa alichukua dhambi za wengi, na kuwaombea wakosaji.
    from verse 50

Where this happens

All Matthew Sites (Jerusalem)
All Matthew Sites (Jerusalem) View full PDF
Matthew 27:45-55
Matthew 27:45-55 View full PDF
The Last Week of Jesus' Life (With Reference Table)
The Last Week of Jesus' Life (With Reference Table) View full PDF

Map © Biblica Open Bible Maps · CC BY-SA 4.0

Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options