Mathayo 24:11-14
11
Watatokea manabii wengi wa uongo, nao watawadanganya watu wengi.
12
Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo wa watu wengi utapoa,
13
lakini yule atakayevumilia hadi mwisho ataokolewa.
14
Injili ya Ufalme itahubiriwa ulimwenguni kote kuwa ushuhuda kwa mataifa yote. Ndipo mwisho utakapokuja.