Mathayo 16:5-7
5
Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate.
6
Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.”
7
Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.”