Mathayo 15:34-38
34
Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mingapi?” Wakamjibu, “Tunayo mikate saba na visamaki vichache.”
35
Yesu akawaambia ule umati wa watu waketi chini.
36
Kisha akachukua ile mikate saba na wale samaki, naye akiisha kumshukuru Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake, nao wakawapa ule umati wa watu.
37
Wote wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu saba.
38
Idadi ya watu walikuwa wanaume 4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto.
Settings