Skip to content
Marko 9:1

Ufalme Waja kwa Nguvu

Marko 9:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Yesu akaendelea kuwaambia, “Amin, nawaambia, kuna watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu ukija kwa nguvu.”
2
Baada ya siku sita, Yesu akawachukua Petro, Yakobo na Yohana, akawapeleka juu ya mlima mrefu, mahali walipokuwa faraghani. Huko, Yesu akageuka sura mbele yao.
3
Mavazi yake yakawa na weupe wa kuzima macho, meupe kuliko ambavyo mtu yeyote duniani angaliweza kuyangʼarisha.
4
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza na Yesu.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options