Marko 7:6-7
6
Yesu akawajibu, “Nabii Isaya alisema ukweli alipotabiri juu yenu, ninyi wanafiki. Kama ilivyoandikwa: “ ‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.
7
Huniabudu bure, nayo mafundisho yao ni maagizo ya wanadamu tu.’