Marko 15:17-19
17
Wakamvalisha Yesu joho la zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamvika kichwani.
18
Wakaanza kumsalimu kwa dhihaka, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
19
Wakampiga kwa fimbo ya mwanzi tena na tena kichwani na kumtemea mate. Wakapiga magoti mbele yake, wakamsujudia kwa kumdhihaki.