Přejít k obsahu
Luka 4:14-19

Luka 4:14-19

14
Kisha Yesu akarudi mpaka Galilaya, akiwa amejaa nguvu za Roho Mtakatifu, nazo habari zake zikaenea katika sehemu zote za nchi za kandokando.
15
Akaanza kufundisha kwenye masinagogi yao, na kila mmoja akamsifu.
16
Yesu akaenda Nazareti, alipolelewa, na siku ya Sabato alikwenda katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama ili asome,
17
naye akapewa kitabu cha nabii Isaya, akakifungua na kukuta mahali palipoandikwa:
18
“Roho wa Bwana yu juu yangu, kwa sababu amenitia mafuta kuwahubiria maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, na vipofu kupata kuona tena, kuwaweka huru wanaoonewa,
19
na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options