Skip to content
Luka 24:39-45

Luka 24:39-45

39
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
40
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
42
Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
43
naye akakichukua na kukila mbele yao.
44
Akawaambia, “Haya ndiyo yale niliyowaambia nilipokuwa bado niko pamoja nanyi, kwamba yote yaliyoandikwa kunihusu mimi katika Sheria ya Mose, Manabii na Zaburi hayana budi kutimizwa.”
45
Ndipo akafungua fahamu zao ili waweze kuyaelewa Maandiko.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options