Luka 24:39-43
39
Tazameni mikono yangu na miguu yangu, mwone kuwa ni mimi hasa. Niguseni mwone; kwa maana mzuka hauna nyama na mifupa, kama mnionavyo kuwa navyo.”
40
Aliposema haya, akawaonyesha mikono na miguu yake.
41
Wakashindwa kuamini kwa ajili ya furaha na mshangao waliokuwa nao. Akawauliza, “Mna chakula chochote hapa?”
42
Wakampa kipande cha samaki aliyeokwa,
43
naye akakichukua na kukila mbele yao.
Settings