Skip to content
Luka 24:13

Luka 24:13

Inaonyesha mstari 13 pamoja na muktadha unaouzunguka.
10
Basi Maria Magdalene, Yoana, na Maria mama yake Yakobo, pamoja na wanawake wengine waliofuatana nao ndio waliwaelezea mitume habari hizi.
11
Lakini hawakuwasadiki hao wanawake, kwa sababu maneno yao yalionekana kama upuzi.
12
Hata hivyo, Petro akainuka na kukimbia kwenda kule kaburini. Alipoinama kuchungulia, akaona vile vitambaa vya kitani, ila hakuona kitu kingine. Naye akaenda zake akijiuliza nini kilichotokea.
13
Ikawa siku iyo hiyo, wanafunzi wawili wa Yesu walikuwa njiani wakienda kijiji kilichoitwa Emau, yapata maili saba kutoka Yerusalemu.
14
Walikuwa wakizungumza wao kwa wao kuhusu mambo yote yaliyotukia.
15
Walipokuwa wakizungumza na kujadiliana, Yesu mwenyewe akaja akatembea pamoja nao,
16
lakini macho yao yakazuiliwa ili wasimtambue.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options