Luka 22:49-51
49
Wafuasi wa Yesu walipoona yale yaliyokuwa yanakaribia kutokea, wakasema, “Bwana, tuwakatekate kwa panga zetu?”
50
Mmoja wao akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa upanga, akamkata sikio la kuume.
51
Lakini Yesu akasema, “Acheni!” Akaligusa lile sikio la yule mtu na kumponya.