Luka 21:1-3
1
Yesu alipoinua macho yake, aliwaona matajiri wakiweka sadaka zao kwenye sanduku la hazina ya Hekalu.
2
Akamwona pia mjane mmoja maskini akiweka humo sarafu mbili ndogo za shaba.
3
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, huyu mjane maskini ameweka humo zaidi ya watu wengine wote.