Skip to content
Luka 20:34-38

Luka 20:34-38

34
Yesu akawajibu, “Katika maisha haya watu huoa na kuolewa.
35
Lakini wale ambao wamehesabiwa kwamba wanastahili kupata nafasi katika ulimwengu ule na katika ufufuo wa wafu, hawaoi wala hawaolewi.
36
Hawa hawawezi kufa tena, kwa maana wao ni kama malaika. Wao ni watoto wa Mungu, kwa sababu ni watoto wa ufufuo.
37
Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila kuteketea, alipomwita Bwana, ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki, na Mungu wa Yakobo.’
38
Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa kuwa kwake wote ni hai.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options