Luka 10:26-28
26
Yesu akamjibu, “Imeandikwaje katika Sheria? Kwani unasoma nini humo?”
27
Akajibu, “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote’; tena, ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.’ ”
28
Yesu akamwambia, “Umejibu vyema. Fanya hivyo nawe utaishi.”
Settings