Luka 10:2-6
2
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili apeleke watendakazi katika shamba lake la mavuno.
3
Haya! nendeni. Ninawatuma kama wana-kondoo katikati ya mbwa mwitu.
4
Msichukue mkoba, wala mfuko, wala viatu, na msimsalimu mtu yeyote njiani.
5
“Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza semeni, ‘Amani iwe kwenu.’
6
Kama kuna mtu wa amani humo, basi amani yenu itakuwa juu yake. La sivyo, itawarudia.
Settings