Yohana 10:7-9
7
Kwa hiyo Yesu akasema nao tena akawaambia, “Amin, amin nawaambia, mimi ndimi lango la kondoo.
8
Wote walionitangulia ni wevi na wanyangʼanyi, lakini kondoo hawakuwasikia.
9
Mimi ndimi lango, yeyote anayeingia zizini kwa kupitia kwangu ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata malisho.