Yohana 10:27-30
27
Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
28
nami ninawapa uzima wa milele, hawataangamia kamwe wala hakuna mtu atakayewapokonya kutoka mikono yangu.
29
Baba yangu aliyenipa hawa ni mkuu kuliko wote na hakuna awezaye kuwapokonya kutoka mikononi mwake.
30
Mimi na Baba yangu tu umoja.”
Settings