Yohana 10:24
Inaonyesha mstari 24 pamoja na muktadha unaouzunguka.
21
Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
22
Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
23
Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
24
Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
25
Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
26
Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
27
Kondoo wangu huisikia sauti yangu nami nawajua, nao hunifuata,
Settings