پرش به محتوا
Yohana 10:23

Yohana 10:23

Inaonyesha mstari 23 pamoja na muktadha unaouzunguka.
20
Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”
21
Wengine wakasema, “Haya si maneno ya mtu aliyepagawa na pepo mchafu. Je, pepo mchafu aweza kufungua macho ya kipofu?”
22
Wakati huo ilikuwa Sikukuu ya Kuwekwa wakfu kwa Hekalu huko Yerusalemu, nao ulikuwa wakati wa majira ya baridi.
23
Naye Yesu alikuwa akitembea ndani ya Hekalu katika ukumbi wa Solomoni.
24
Wayahudi wakamkusanyikia wakamuuliza, “Utatuweka katika hali ya mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo tuambie waziwazi.”
25
Yesu akawajibu, “Nimewaambia, lakini hamwamini. Mambo ninayoyatenda kwa jina la Baba yangu yananishuhudia.
26
Lakini hamwamini, kwa sababu ninyi si wa kundi la kondoo wangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options