Ayubu 38:1-7
1
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Settings