Skip to content
Ayubu 33:14-22

Ayubu 33:14-22

14
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options