Ayubu 30:22
Inaonyesha mstari 22 pamoja na muktadha unaouzunguka.
19
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Settings