Ayubu 11:15-19
15
ndipo utainua uso wako bila aibu; utasimama imara bila hofu.
16
Hakika utaisahau taabu yako, utaikumbuka tu kama maji yaliyokwisha kupita.
17
Maisha yako yatangʼaa kuliko adhuhuri, nalo giza litakuwa kama alfajiri.
18
Utakuwa salama, kwa kuwa lipo tumaini; utatazama pande zote na kupumzika kwa salama.
19
Utalala, wala hakuna atakayekuogofya, naam, wengi watajipendekeza kwako.
Settings