Aller au contenu
Ayubu 10:2-7

Ayubu 10:2-7

2
Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
3
Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
4
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
5
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
6
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
7
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options