Yakobo 2:17-20
17
Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.
18
Lakini mtu mwingine atasema, “Wewe unayo imani; mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo.
19
Unaamini kwamba kuna Mungu mmoja. Vyema! Hata mashetani yanaamini hivyo na kutetemeka.
20
Ewe mpumbavu! Je, wataka kujua kwamba imani bila matendo haifai kitu?
Settings