Skip to content
Yakobo 2:14-19

Yakobo 2:14-19

14
Ndugu zangu, yafaa nini ikiwa mtu atadai kuwa anayo imani lakini hana matendo? Je, imani kama hiyo yaweza kumwokoa?
15
Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula,
16
mmoja wenu akamwambia, “Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,” pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini?
17
Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.
18
Lakini mtu mwingine atasema, “Wewe unayo imani; mimi ninayo matendo.” Nionyeshe imani yako pasipo matendo nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo.
19
Unaamini kwamba kuna Mungu mmoja. Vyema! Hata mashetani yanaamini hivyo na kutetemeka.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options