Isaya 24:7-12
7
Divai mpya inakauka na mzabibu unanyauka, watu wote wafurahishao wanalia kwa huzuni.
8
Furaha ya matoazi imekoma, kelele za wenye furaha zimekoma, shangwe za kinubi zimenyamaza.
9
Hawanywi tena mvinyo pamoja na wimbo, kileo ni kichungu kwa wanywaji wake.
10
Mji ulioharibiwa umekuwa ukiwa, mlango wa kila nyumba umefungwa.
11
Barabarani wanalilia kupata mvinyo, furaha yote imegeuka kuwa majonzi, furaha yote imefukuziwa mbali na dunia.
12
Mji umeachwa katika uharibifu, lango lake limevunjwa vipande.
Settings