Isaya 19:8-10
8
Wavuvi watalia na kuomboleza, wale wote watupao ndoano katika Mto Naili, watadhoofika kwa majonzi.
9
Wale watu wafanyao kazi ya kitani kilichochambuliwa watakata tamaa, wafumaji wa kitani safi watavunjika moyo.
10
Wafanyao kazi ya kufuma nguo watahuzunishwa, nao vibarua wataugua moyoni.