Skip to content
Isaya 19:5-10

Isaya 19:5-10

5
Maji ya mito yatakauka, chini ya mto kutakauka kwa jua.
6
Mifereji itanuka; vijito vya Misri vitapungua na kukauka. Mafunjo na nyasi vitanyauka,
7
pia mimea iliyoko kando ya Mto Naili, pale mto unapomwaga maji baharini. Kila shamba lililopandwa kando ya Mto Naili litakauka, litapeperushwa na kutoweka kabisa.
8
Wavuvi watalia na kuomboleza, wale wote watupao ndoano katika Mto Naili, watadhoofika kwa majonzi.
9
Wale watu wafanyao kazi ya kitani kilichochambuliwa watakata tamaa, wafumaji wa kitani safi watavunjika moyo.
10
Wafanyao kazi ya kufuma nguo watahuzunishwa, nao vibarua wataugua moyoni.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options