Isaya 13:7-8
7
Kwa sababu ya hili, mikono yote italegea, moyo wa kila mtu utayeyuka.
8
Hofu itawakamata, uchungu na maumivu makali yatawashika, watagaagaa kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa. Watatazamana kwa hofu kila mtu na mwenzake, nyuso zao zikiwaka kama moto.