Hosea 13:9-11
9
“Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
10
Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
11
Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
Settings